Jumanne, 2 Desemba 2014

NATO yajadili "mwaka wa uchokozi"


Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO wanakutana leo mjini Brussels kutathmini mkakati wa pamoja, baada ya kile wanachokiita "mwaka wa uchokozi" nchini Ukraine na Mashariki ya Kati na pia kujadili kumalizika kwa kampeni yao ya kijeshi nchini Afghanistan. Mawaziri hao pia watajadili juhudi za NATO kuwahakikishia usalama wao wanachama wake wa mataifa ya mashariki mwa Ulaya, mukiwemo doria ya ndege za kijeshi, meli na wanajeshi wa ardhini. Mkuu mpya wa NATO, Jens Stoltenberg, amesema mkutano huu unakuja wakati Urusi ikiwa imejiingiza Ukraine na kitisho cha kundi lijiitalo Dola la Kiislamu kikiendelea nchini Iraq na Syria, na kwamba mwaka 2014 umekuwa mwaka wa uchokozi, migogoro na mizozo. Mwezi Septemba mwaka huu, viongozi wa mataifa 28 wanachama wa NATO, walikubaliana kuunda kikosi cha dharura kukabiliana na changamoto zisizotegemewa, wakisema sasa wanakabiliwa na kitisho kipya kwa usalama wa eneo lao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni