Jumatano, 10 Desemba 2014

Cameron atoa heshima zake kwa wahanga wa kambi ya Auschwitz

Waziri mkuu wa Uingereza  David Cameron  leo ametoa heshima zake kwa wahanga  wa  mauaji  ya Holocaust  katika kambi  ya mateso ya utawala  wa Wanazi  wa Ujerumani wakati wa vita  vikuu vya pili vya dunia  ya Auschwitz, ambayo hivi sasa ni  makumbusho kusini mwa Poland.
Cameron  ametembelea  kambi  hiyo  na  baadaye aliangalia maonesho  juu  ya  wahanga. Kiongozi  huyo  wa  Uingereza alisimama  kwa  muda  nchini  Poland  baada  ya  kuizuru  Uturuki kuangalia  kambi  hiyo  kwa  mara  ya  kwanza.
Cameron  amesema  hatupaswi  kuwasahau  wale  wote waliouwawa  katika  kambi  hiyo na  kambi  nyingine, na  kila  mara tunapaswa  kukumbuka  kile  kilichotokea.
Auschwitz - Birkenau imekuwa  ishara ya  mauaji  ya  halaiki  ya Wanazi  wa  Ujerumani  dhidi  ya  Wayahudi  wa  Ulaya , ambapo milioni  moja  wameuwawa  katika  kambi  hiyo  kuanzia  mwaka 1940 hadi  1945. Kwa  mujibu  wa  makumbusho  hiyo zaidi  ya  watu wengine  100,000 ikiwa  ni  pamoja  na  Wapoland  ambao  si Wayahudi, Waroma, wafungwa  wa  kivita  wa Kirusi  na  waliokuwa wakipinga  utawala  wa  Kinazi pia  wameuwawa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni