Jumatano, 10 Desemba 2014

Mugabe amteua Munangagwa makamu wa rais

Rais  Robert  Mugabe  wa  Zimbabwe  amemteua  waziri  wa  sheria Emmerson  Munangagwa kuwa  makamu  wake  mpya   katika chama  tawala  cha  ZANU-PF na  serikali  ya  nchi  hiyo leo, katika hatua  ambayo  imekuwa  ikitarajiwa  baada  ya  kumfuta  kazi makamu  wake Joice Mujuru.
Kiongozi  huyo  wa  muda  mrefu  pia  amemteua  mwanadiploamsia wa  zamani Phelekezela Mphoko  kuwa  makamu  wa  pili  wa  rais na  kusema  viongozi  hao  wawili  wataapishwa  siku  ya  Ijumaa.
Taarifa  iliyotolewa  na  serikali  jana  imesema  rais  Mugabe amewafuta  kazi  mawaziri  wake  wanane  kwa  kuhusika  na  madai ya  rushwa ikiwa  ni  pamoja  na  Joice Mujuru  ambaye  ni  makamu wake  wa  rais.
Walioondolewa  katika  nyadhifa  zao ni pamoja  na  washirika  wa Joice Mujuru  katika  wizara  za  nishati, huduma  za  umma , na wengine  sita  katika  idara  nyingine.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni